• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Mtwara District Council
Mtwara District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya sekondari
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Maji na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kazi na Kikosi cha Zima Moto.
      • Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Vijana
      • Ardhi,Maliasiri na Mazingira
      • Utawala
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kililmo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano.
    • Kamati za Halmashauri
      • Kamati ya Elimu,Afya na Maji
      • Kamati ya Fedha,Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi,Kazi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Uwekezaji
    • Agriculture
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za kijamii
    • Huduma za Kifedha
    • Usambazaji Nishati ya Umeme
    • Maji
  • Madiwani
    • Kata ya Nanguruwe
    • Kata ya Mbawala
    • Kata ya Naumbu
    • Kata ya Ziwani
    • Kata ya Libobe
    • Kata ya Mayanga
    • Kata ya Ndumbwe
    • Kata ya Dihimba
    • Kata ya Mkunwa (HQ)
  • Miradi
    • Miradi Mpya
      • On going Project
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Zabuni
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio

Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji

IDARA YA MIPANGO, TAKWIMU NA UFUATILIAJI

1.0 UTANGULIZI;

Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji ni kiungo cha Idara zote katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara. Idara hii inahusika katika usimamizi wa uandaaji wa Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP), maelezo mafupi ya Halmashauri, (Social profile), maelezo mafupi ya uwekezaji (Investment Profile) pamoja na Mpango na Bajeti ya kila mwaka. Idara pia inahusika katika Ukusanyaji na uchambuzi wa Takwimu mbalimbali za kiuchumi na kijamii katika Halmashauri ya Wilaya. Aidha, utekelezaji wa mpango na bajeti kwa kila mwaka husimamiwa na idara hii kwa kushirikiana na Idara zote. Idara hii inaongozwa na Afisa Mipango wa Wilaya na imegawanyika katika sehemu tatu kama ifuatavyo:-

  • Mipango na Sera.
  • Usimamizi na Ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo.
  • Tafiti na Takwimu.

MAJUKUMU MUHIMU YA IDARA.

Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji ina jukumu la kuratibu utoaji wa taarifa mbalimbali za maendeleo za Wilaya kwa Viongozi wa ngazi za Kitaifa, Kimkoa, Wilaya na wadau wa maendeleo, pamoja na kazi zingine za kawaida ina majukumu muhimu yafuatayo;

  1. Kuandaa, kusimamia na kuratibu shughuli zote za kazi katika utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wilaya.
  2. Kufuatilia utekelezaji wa Sera mbalimbali za kisekta na kutoa ushauri.
  3. Uratibu na utayarishaji wa Mipango shirikishi katika Kata zote za Halmashauri kupitia Mfumo wa fursa na vikwazo kwa maendeleo (O&OD).
  4. Kusimamia uandaaji wa mipango kazi (Action Plans) ya bajeti za kila mwaka na  kuziwasilisha katika ngazi husika.
  5. Kuandaa na kuratibu uandaaji wa maandiko ya miradi mbalimbali ya maendeleo na kuwasilisha kwa wadau mbalimbali wa maendeleo.
  6. Kusimamia na kuratibu Utekelezaji wa Maagizo mbalimbali ya Viongozi wa Kitaifa, Mkoa na Wilaya.
  7. Kukusanya, kuchambua na kupanga takwimu zinazohusu mipango ya kijamii na kiuchumi katika Wilaya.
  8. Kusimamia tafiti ndogondogo za maeneo muhimu ili kupata hali halisi ya kupanga program za maendeleo.
  9. Kiungo cha sekta zote juu ya kubuni, kupanga, kutekeleza na kutathmini kiufanisi miradi ya maendeleo na kuweka kipaumbele cha shughuli zitakazotekelezwa kulingana na matakwa ya Nchi, Mkoa na Wilaya.
  10. Kuratibu, kusimamia na kubainisha maeneo muhimu ya uwekezaji kwa kushirikiana na Sekta mbalimbali ndani ya Halmashauri.
  11. Usimamizi, ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi ya  maendeleo katika Wilaya.
  12. Kukusanya, kuchambua na kusimamia benki ya Takwimu ya Halmashauri ikihusisha mifumo yote ya  takwimu.

3.0 ORODHA YA WATUMISHI

         Idara ina  jumla ya watumishi 04 kama ifuatavyo:-       

          Mkuu wa Idara                      1

         Wachumi                                2

          Mtakwimu                             1

 

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA BAJETI YA MWAKA  2016/2017.

A: UTANGULIZI,

Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ilipanga kukusanya na kutumia jumla ya shilingi 6,818,086,000.00 katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2016/2017.  Sawa na asilimia 23.6 ya bajeti nzima ya Halmashauri ya Wilaya inayofikia shilingi 28,770,100,000.00

Mchanganuo wa fedha hizo za maendeleo na vyanzo vyake ni kama unavyoonekana katika jedwali hapa chini:-

 NA 
 CHANZO 

 KIASI 

 % 

   1
 Mapato ya ndani (Own Source)

1,334,956,000.00

17.6

   2
 Ruzuku serikali kuu

5,440,130,000.00

81.7

   3
 Wadau wa maendeleo

43,000,000.00

0.7

 
 JUMLA 

6,818,086,000.00

100.0

B: MAPATO, 

Halmashauri ya Wilaya imeshapokea kiasi cha shilingi 5,917,546,329.58 sawa na asilimia 78.3 tu ya makisio ya mwaka 2016/2017 zikiwa ni kwa ajili ya kunusuru Kaya maskini (TASAF III), Maji, Mfuko wa barabara, UNICEF na LGCDG.

 

C: MATUMIZI,

Hadi sasa kiasi cha shilingi 4,877,939,074.57 kimeshatumika kugharamia miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya  Wilaya Mtwara.

 

 

 

 

 

 

D: UTEKELEZAJI,

Na

SEKTA

JINA LA MRADI

HALI YA UTEKELEZAJI

01.
Elimu ya Sekondari
Ujenzi wa vyumba vya maabara 33
Ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule za Sekondari 11 upo katika hatua ya umaliziaji.
Utengenezaji wa madawati
Jumla ya madwati 900 yametengenezawa na kuyapeleka katika shule zote za sekondari.
Ujenzi wa matundu ya vyoo.
Ujenzi wa matundu ya vyoo 10 katika shule ya sekondari Libobe na 10 Ndumbwe umefanyika.
Ujenzi wa vyumba vya madarasa
Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa katika sekondari ya Madimba unaendelea.
02.
Elimu ya Msingi
Ujenzi wa vyumba vya madarasa
Ujenzi wa vyumba vya madarasa 8 umekamilika katika shule ya Mbawala na madarasa 3 katika shule za msingi Mnomo, Ilala na Nanyati unaendelea.
Utengenezaji wa madawati
Jumla ya madawati 200 yametengenezwa.
Ujenzi wa matundu ya vyoo
Ujenzi wa matundu ya vyoo 18 umekamilika katika shule ya Mbawala na matundu 15 katika shule za Mnete, Utende na Kitunguli unaendelea.
Ujenzi wa nyumba za walimu
Ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi Mtandi umekamilika.
03.
Afya
Ujenzi wa Zahanati mpya
Ujenzi wa nyumba 4 katika OPD mpya zilizo katika vijiji vya Makome A, Makome B, Mtama na Nanyani upo katika hatua za awali.

Ujenzi wa OPD katika vijiji vya Mbuo, Mngoji na Likonde unaendelea.
04.
Maji
Mradi wa maji Msangamkuu
Ukamilishaji wa ujenzi wa mradi huu unaendelea na umefikia asilimia 85 ya ukamilishaji.
Mradi wa maji Kilambo
Ukamilishaji wa ujenzi wa mradi huu unaendelea na umefikia asilimia 85 ya ukamilishaji.
Mradi wa maji Mpapura - Lyowa
Ukamilishaji wa ujenzi wa mradi huu unaendelea na umefikia asilimia 70 ya ukamilishaji.
Mradi wa maji Mayaya
Ukamilishaji wa ujenzi wa mradi huu unaendelea na umefikia asilimia 70 ya ukamilishaji.
05.
Barabara
Matengenezo ya dharura ya barabara
Ujenzi wa kalvati mistari minne pamoja na kuta na mikono ya kalvati imejengwa katika barabara ya Chekeleni – Mkonye hadi Mtama, kazi imekamilika.
Ujenzi wa daraja
Uchimbaji wa msingi wa daraja,ujenzi wa nguzo tatu za daraja,ujenzi wa kuta za mikono ya daraja na kumimina zege  la deki ya daraja katika barabara ya Namuhi-Mnyija  kazi imekamilika.
06
Kilimo
Ujenzi wa bwawa na mifereji ya umwagiliaji
Ujenzi wa bwawa na mifereji ya umwagiliaji katika mradi wa umwagiliaji Kitere unaendelea na umefikia asilimia 95 ya ukamilishaji.
07
Mfuko wa  Jimbo
Ununuzi wa  saruji
Mifuko 2,050 ya saruji imenunuliwa kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maendeleo, saruji imeshapelekwa
08
TASAF
Kusaidia kaya 10,449 kujikwamua na umaskini
Jumla ya kaya 10,129 maskini zimewezeshwa na  jumla ya Tsh 1,361,699,650.40 zimetumika.
09
Maendeleo ya Jamii
Kuwezesha utoaji wa mikopo
Jumla ya vikundi 33 vya wanawake na vijana vimepewa mkopo wa jumla ya Tsh  62,740,000 kutoka kwenye vyanzo vya ndani vya mapato ya Halmashauri

 

Responsibilities of Planning, Monitoring and Statistics Department in Mtwara DC

  • Coordinate the activities of the Council budget preparation

  • Coordinate the preparation of the implementation of the strategic plan of the Council

  • Coordinate the activities of collection, analysis, and interpretation of the data handling various newspapers to make use especially in planning development projects.

  • Coordinate the activities of the implementation of the development projects of the District ventures, aviation projects

  • Prepare labels of various projects (project write ups) for the purposes of pointers to pray for funding from various donors.

  • Coordination of participatory community planning activities

  • Secretary of the committee of the Council Expert

  • Secretary of the Economic Committee, Construction and Environment

  • Coordinate the review of the reporting process of the District (District Profile) for example: Social Economic Profile, etc. Investment Profile

  • Coordinate the preparation of the action plan election manifesto with its reports on the implementation (of the half year and full year).

  • Provide advice on economic issues and raising the output of resident to strengthen modern agriculture and animal husbandry as well as other economic activities.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI KWA WALIOFAULU USAILI January 18, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KUKIMBIZA MWENGE WA UHURU April 11, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI DAFTARI LA MPIGA KURA 2024 January 09, 2025
  • TANGAZO LA UCHAGUZI September 16, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MHE. SAWALA AWATAKA WAFANYAKAZI WA MTWARA KUIPENDA MTWARA

    May 01, 2025
  • DED KAFUNDA AWAASA MAAFISA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NGAZI YA KATA KWENDA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    January 22, 2025
  • KATIBU WA CCM MKOA WA MTWARA APONGEZA USIMAMIZI WA MIRADI YA ZAIDI YA MILIONI 800 MTWARA DC

    January 07, 2025
  • KATIBU WA CCM MKOA WA MTWARA APONGEZA USIMAMIZI WA MIRADI YA ZAIDI YA MILIONI 800 MTWARA DC

    January 07, 2025
  • Angalia Zote

Video

RC Mtwara ataka mabadiliko Ligula Hospitali
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • New Projects
  • Speeches
  • Organizational Structure
  • Tenders
  • Applications Forms

Kurasa Mashuhuri

  • Tanzania Government Website
  • PO-RAG
  • Public Service Management
  • Mtwara Region Office
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Mtwara.

    Anuani ya posta: 528.

    Simu ya Mezani: 023-2333928

    Simu: 023-2333928

    Barua pepe: dedmtwara@mtwaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2023 MTWARA DC . All rights reserved.