• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Mtwara District Council
Mtwara District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya sekondari
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Maji na Umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kazi na Kikosi cha Zima Moto.
      • Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Vijana
      • Ardhi,Maliasiri na Mazingira
      • Utawala
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kililmo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano.
    • Kamati za Halmashauri
      • Kamati ya Elimu,Afya na Maji
      • Kamati ya Fedha,Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi,Kazi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Uwekezaji
    • Agriculture
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za kijamii
    • Huduma za Kifedha
    • Usambazaji Nishati ya Umeme
    • Maji
  • Madiwani
    • Kata ya Nanguruwe
    • Kata ya Mbawala
    • Kata ya Naumbu
    • Kata ya Ziwani
    • Kata ya Libobe
    • Kata ya Mayanga
    • Kata ya Ndumbwe
    • Kata ya Dihimba
    • Kata ya Mkunwa (HQ)
  • Miradi
    • Miradi Mpya
      • On going Project
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Zabuni
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio

Wanaoanzisha migogoro ardhi wapigwa “stop"

Posted on: July 6th, 2020


Na. Afisa habari

Wananchi katani msimbati halmashauri ya wilaya ya mtwara siku ya ijumaa 03 Julai, 2020 wamezuiwa jaribio lao la kuanzisha mgogoro wa kutaka kudai fidia serikalini kutokana na kutwaliwa eneo ilipojengwa shule ya sekondari msimbati.

Zuio hilo limetolewa na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Ndg. Gelasius G. Byakanwa alipokuwa anatoa majibu ya hoja mbalimbali zilizotolewa na wananchi wakati wa mkutano wa hadhara kushughulikia kero katani msimbati ambapo walitaka kujua serikali italipa lini fidia ya mazao yaliyokuwa katika eneo la shule kwakuwa umepita muda mrefu.

Akitolea maelezo hoja hiyo, mkuu wa mkoa alieleza kuwa, utaratibu unaotumika kutwaa maeneo kwaajili ya ujenzi wa sekondari za kata unafahamika, inatolewa na serikali ya kijiji kwa ridhaa ya wananchi kisha ujenzi unaendelea na hatua zote zinafuata taratibu za kisheria.

Aliongeza kuwa, wanufaika wakubwa wa huduma ya elimu ni watoto wanaotokana na jamii ambayo iliamua kutoa eneo husika kama ilivyojidhihirisha kwa baadhi ya vijana waliotoa michango yao kwenye mkutano huo, wameonesha kutoa michango mizuri sana.

Aliendelea kusema kuwa haoni asili ya mgogoro hapo isipokuwa kwa wale watakaoamua kujitoa ufahamu nje ya utaratibu uliotumika, ndiyo maana kuna mwananchi mwenzao ametoa maelezo mazuri sana yanayofanana na utaratibu wa kisheria uliotumika kutwaa eneo hilo na amethibitisha kuwa ridhaa ilitoka kwao wenyewe hayo mazao yamepandwa baada ya shule kuwepo.

Historia inaeleza kuwa eneo hilo lilitolewa na kijiji mwaka 1994 ili kuruhusu ujenzi wa shule ya sekondari, mara baada ya taratibu zote kufuatwa ujenzi ulifanyika na mwaka 2004 shule ikaanza kuchukua wanafunzi ambapo zaidi ya miongo miwili na nusu hakujawahi kutokea mgogoro, ila kwa sasa wameibuka watu wasiotaka kukubaliana na uhalisia.

Kutokana na maelezo hayo ya kutosha, iliagizwa kuwa eneo lote la shule liheshimiwe, litunzwe hakuna ruhusa kwa mwananchi yeyote kufanya shughuli zake, pia wataalamu wa ardhi wametakiwa kubainisha mipaka ya eneo husika ili kuondoa uwezekano wa wavamizi ambapo zoezi hilo limetakiwa kufanywa kwa maeneo yote ya taasisi za serikali.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE USAILI February 01, 2021
  • MABADILIKO YA UKUMBI WA KUFANYIA USAILI February 03, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Mtwara DC kufungua sekondari 4 mpya Januari Mwakani

    December 07, 2020
  • Wanaoanzisha migogoro ardhi wapigwa “stop"

    July 06, 2020
  • Naumbu Msangamkuu zanufaika ziara ya DC

    July 01, 2020
  • Halmashauri yapewa wiki mbili kukamilisha madarasa 15

    June 27, 2020
  • Angalia Zote

Video

RC Mtwara ataka mabadiliko Ligula Hospitali
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • New Projects
  • Speeches
  • Organizational Structure
  • Tenders
  • Applications Forms

Kurasa Mashuhuri

  • Tanzania Government Website
  • PO-RAG
  • Public Service Management
  • Mtwara Region Office
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Mtwara.

    Anuani ya posta: 528.

    Simu ya Mezani: 023-2333928

    Simu: 023-2333928

    Barua pepe: Mtwaradc@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2020 MTWARA DC . All rights reserved.